Na Muandishi wetu
Walimu polisi 48 wa
Mikoa mitatu ya Unguja wanapatiwa mafunzo ya somo la Usalama wetu kwanza,
ambalo litakuwa likifundishwa kwa wanafunzi wa skuli za msingi ili kukabiliana
na vitendo vya udhalilishaji.
Akifungua mafunzo
hayo ya wiki moja, Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto, Abeda Rashid amesema somo hilo litasaidia kuibua taarifa za vitendo vya
udhalilishaji ambazo hazijaripotiwa katika vituo vya polisi.
Aidha ameipongeza
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa kuruhusu kutolewa kwa somo hilo katika
skuli mbalimbali nchini.
Nae Kamanda wa
polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, ACP Richard Mchomvu amesema asilimia 80 ya
makosa ya udhalilishaji yanatokana na watoto wenyewe kujiingiza katika mapenzi
hivyo wakipatiwa mafunzo hayo itadaidia kupunguza makosa hayo.
Awali Mratibu wa
program ya Malezi mbadala kutoka SOS, Nyezuma Simai amesema wameamua kutoa
mafunzo hayo kwa walimu polisi ili kuwajengea uwezo wa kufundisha haki, wajibu
wa mtoto pamoja na kuvitambua na kujilinda na vitendo vya udhalilishaji.
0 Maoni