Na Mundishi wetu Kidawa
Mkutano wa 11 wa baraza la kumi la wawakilishi
Zanzibar unatarajiwa kuanza jumatano ya tarehe 10 mei 2023 saa 3:00 asubuhi.
Katibu wa baraza la
wawakilishi raya issa mlsellem ametoa taarifa hiyo wakati akizungumza na
waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari katika ofisi za baraza hilo huko
chukwani Zanzibar.
Raya amefahamisha kuwa Mkutano
huo utahusisha maswali na majibu ambapo afisi ya baraza la wawakilishi imepokea
na kuratibu maswali 246.
Amesema baraza hilo pia
litahusisha majadiliano ya bajeti ya serikali ya mapinduzi Zanzibar kwa mwaka
wa fedha 2023/2024.
Amesema katika mikutano
huo pia miswaada minne ya sheria itawasilishwa ikiwemo mswaada wa sheria wa fedha,
Mswada
wa sheria ya kuidhinisha matumizi ya serikalikwa mwaka 2023/2024,
Mswada
wa kufuta sheria ya kuzuia rushwa na kuhujumu uchumi Zanzibar namba 1 ya mwaka 2012 kutunga upya sheria sheria ya
kuzuia rushwa na kuhujumu uchumi Zanzibar na mambo mengine yanayohusianana na
hayo.
0 Maoni