Na Muandishi wetu Donald Martin
Bodi ya Bima ya Amana (DIB) imesema mkwamo uliokuwa
ukitatiza mchakato wa ufilisi wa iliyokuwa benki ya FBME Tanzania tawi la
Cyprus umetatuliwa.
Mkurugenzi wa DIB, Isack Kihwili amesema Disemba 12,
2022 Serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia DIB ilifikia
makubaliano na benki kuu ya Cyprus kuhusiana na ufilisi wa tawi la FBME Cyprus.
Amesema baada ya changamoto ndogo ndogo za kisheria
kuwekwa sawa ufilisi wa tawi la Cyprus utaanza rasmi na baada ya hapo waliokuwa
wateja wa benki hiyo watalipwa stahiki zao.
0 Maoni