Na muandishi wetu
Mkurugenzi Mkuu wa
Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC, Dkt. Samuel Gwamaka
amesema jumla ya baa na kumbi za starehe 89 zimefungiwa baada ya kubaini kupiga
kelele na mitetemo iliyozidi viwango vinavyotakiwa.
Hatua hiyo imekuja
baada ya NEMC kwa kushirikiana na jeshi la polisi kufanya msako katika majiji
ya Dar es salaam, Mwanza na Dodoma kubaini baa na kumbi za starehe zinazopiga
muziki kwa sauti ya juu ambayo ni kinyume cha sheria ya mazingira ya mwaka
2014.
Dkt. Gwamaka
amesema wamezifungia baa na kumbi hizo za starehe kwakuwa sio mara ya kwanza
kutenda makosa hayo licha ya kuonywa pamoja na kutozwa faini na NEMC.
Baa na kumbi za starehe
zilizofungiwa ni 19 kutokea Kinondoni, 25 Ilala, 22 za Kigamboni na Temeke 12,
Jijini Dodoma tano na 48Mwanza sita.
0 Maoni