Na muandishi wetu
Wizara ya Uchumi wa
Bluu Zanzibar, imekabidhi Boti 32 za Uvuvi kwa Wavuvi na Wakulima wa Mwani
pamoja na Mabwawa ya kisasa kwa Wafugaji wa Mazao ya Bahari Kisiwani Pemba
Akizungumza na Wajasiriamali, katika hafla ya
ugawaji wa Vifaa hivyo, katika Afisi za Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi
Pemba, Waziri wa Wizara hiyo, Mh. Suleiman Masoud Makame, Amesema Serikali
imekusudia kunyanyua Wananchi wake kiuchumi hivyo amewataka Wajasiriamali,
kuzitumia Boti hizo ili kufikia malengo pamoja na kuendelea kuitunza Bahari..
Mkurugenzi Mipango,
Sera, na Utafiti, Wizara ya Uchumi wa Bluu Zanzibar, Sheha Idrisa Hamdan na
Mkuu wa Wilaya ya Wete, Nd. Hamad Omar Bakar, wamesema ni imani ya Serikali
baada ya kutolewa Vifaa hivyo kipato cha Wananchi kitaongezeka..
Vifa hivyo
vilivyokabidhiwa vimegharimu Kiasi cha Shilingi Bilioni 1 kutoka katika Mfuko
wa Ahuweni 19, kwa ushirikiano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na
Benk ya CRBK..
0 Maoni