Namwandishi wetu

   

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe: Rashidi Hadidi Rashidi amewataka Wananchi wa Mkoa wa Kusini kuendelea kudumisha Muungano wa Tanganyika na Zanizibar ili kulinda amani na mshikamano uliopo Nchini.

Akizungumza katika kilele cha kuadhiimisha Muunganono ,huko katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) Tunguu,  amesema Muungano huo ulio dumu kwa  Miaka 59,umekua chachu ya kuleta maendeleo katika Taifa ikiwemo Afya, elimu, maji safi na salama na miundombinu ya barabara.

Amesema hata hivyo katika kuadhimisha miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Wananchi wa Mkoa huo wanakila sababu ya kutathmini misingi iliyoachwa na Waasisi wa Muungano ili iendelee kuimarisha umoja,amani na utulivu wa taifa letu.

Nae  Mkuu wa Wilaya ya Kusini  Rajab Yussuf Mkasaba ameahidi kupitia Wananchi wa Wilaya ya Kati na Kusini  kuenzi na kuulinda Muungano kwa ajili ya kuleta maendeleo

Akitoa neno la shukurani kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa Ndg: Makame Ramadhan Makame amesema kupitia kauli mbiu ya Muungano huo  Chama cha Mapinduzi kitaendelea kutoa Elimu ya kuutunza  pamoja na kuwaenzi waasisi wa muungano.

Itakumbukwa kuwa kila ifikapo tarehe 26/4 serikali huadhimisha sherehe hizo kitaifa ambapo kwa mwaka huu sherehe hizo zimefanyika kimkoa ambapo kauli mbiu ni   “umoja na mshikamano ndio nguzo ya kukuza uchumi wetu”.