Na muandishi wetu

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Mhe Haroun Ali Suleiman amesema ipo haja ya kuendelea kuielimisha jamii hususan vijana ili waweze kuijua vyema historia ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ili kuepusha upotoshwaji wa historia hiyo.

Ametoa kauli hiyo wakati akizindua kongamano la kuadhimisha miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar (ZU) Kibele Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja,

Amesema hatua hiyo itawaongezea  uelewa pamoja na kuyajua mafanikio yaliopatikana kutokana na ushirikiano mzuri baina ya pande mbili za Muungano.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Rashid Hadidi Rashid amesema kongamano hilo limekuja ili kuwapa elimu vijana kutokana na kuwa vijana wengi hawajui historia ya muungano.

Kwa upande wake, Muhadhiri muandamizi chou cha Uandishi wa Habari Zanzibar, Ali Shaaban Juma amewataka wasomi kufanya tafiti na kuandika kwa kina juu ya muungano wa Zanzibar na Tanganyika ili kuwa na historia yenye  taarifa sahihi.

Nao baadhi ya Vijana walioshiri katika kongamano hilo wameahidi kwenda kuwaelimisha vijana wenzao juu ya elimu waliyoipata kwenye kongamano hilo.

Kongamano hilo la siku moja lililowashirikisha viongozi wa chama cha mapinduzi   wa Mkoa wa Kusini unguja  , mabaraza ya vijana pamoja na wanafunzi wa vyuo vikuu ambapo mada ya kuhusu historia na faida ya Muungano.