Mkuu wa mkoa wa kusini unguja Mh: Rashid Hadid
Rashi amesema katika kuadhimisha Miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar Serikali ya Mkoa wa Kusini unguja imeandaa Kongamano kubwa
litakaloweza kutoa Elimu kwa Umma kuelewa juu ya tunu ya Muungano.
Akizungumza na Vyombo vya Habari huko Ofisini
kwake Tunguu Mkuu huyo amesema hatua hiyo itasaidia Wananchi hususan Vijana
kuelewa Historia na Faida ya Kuunganishwa kwa Nchi hizi mbili
sambamba na kufahamu maendeleo yaliopo katika Muungano huo na kuzitumia ipasavyo
Fursa mbali mbali zilizopo ikiwemo za Kiuchumi, Kisiasa na Kijamii.
Akizungumzia Miaka 59 ya Muungano huo Mh: Rashid
amesema ndani ya kipindi hicho Mkoa huo umepata Mafanikio mbali mbali ikiwemo
kutekelezwa kwa Miradi Mbalimbali ya kimaendeleo kama vile Majengo ya Kisasa,
Miundombinu ya Barabara pamoja na Maji Safi na Salama .
Aidha amesema kwa Mkoa huo Sherehe hizo
zimeanza kwa Shuhuli za Usafi katika Maeneo mbali mbali ya Mkoa huo, Dua na
Sala pamoja na Mpira wa Miguu ambapo kilele chake kitafanyika Ukumbi wa Dk: Ali
Muhammed Shein Tunguu huku akiwataka Wananchi kujitokeza kwa wingi katika Sherehe
hizo.
Sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
huadhimishwa kitaifa kila ifikapo Tarehe 26 April ambapo kwa Mwaka huu Sherehe
hizo zinafanyika Kimkoa ikiwa ni agizo la Mh: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dk; Samia Suluhu Hassan.
0 Maoni