Na mwandishi wetu
Mkuu wa Wilaya ya
Kusini Unguja Bw. Rajab Yussuf Mkasaba ameitaka Jamii kuacha kuwafanyia vitendo
vya Udhalilishaji watoto wenye ulemavu kwa kuwafungia Ndani kwani kufanya
hivyo ni kuwanyima haki zao za Msingi.
Akifunguwa kongamano la Wadau
wa Maendeleo Jumuishi katika jamii (Cbid) huko Ofisi ya Mkoa Tunguu, Mkasaba amesema
kila mmoja ni Mlemavu mtarajiwa hivyo kitendo cha kuwafungia ndani watu wenye
Ulemavu ni kosa na halikubaliki katika Jamii kwani kufanya hivyo ni kwenda
kinyume na haki za binaadamu.
Katibu Mtendaji Baraza
la Taifa la Watu Wenye Ulemavu Zanzibar Khamis Ussi Debe amesema baraza kwa
kushirikiana na Taasisi ya Madrasa Early Childhood wameweza kuwahamasisha watu
wenye ulemavu kutetea haki zao, huku wakiwa tayari kuzungumza changamoto zinazo
wakabili.
Nao baadhi ya
washiriki katika Kongamano hilo wakazungumzia hali ya Watu wanaowatumia watu
wenye Ulemavu kuwa omba omba kwa maslahi yao, hivyo wameiomba Serikali kuwachukulia
hatua zinazofaa.
Kongamano la wadau (Cbid) lililoanadaliwa na Taasisi ya Madrasa Early Childhood kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu lenye kauli Mbiu "Hakuna Linalotuhusu Sisi Pasi Na Sisi" na kuwashirikisha Masheha Wa Wilaya Ya Kusini, wadau wa watu wenye ulemavu kwa lengo la kujadili changamoto na kuzitafutia ufumbuzi.
0 Maoni