Na muandishi wetu

Waumini wa Dinini ya Kiislamu na Madhehebu mengine kutoka Mkoa wa Kusini Unguja wameunganakwa  pamoja katika dua na sala ya kuliombea taifa la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ili nchi izidi kuendelea kuwa na amani na utulivu.

 

Dua hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) Tunguu wilaya ya Kati ni miongoni mwa muendelezo wa maadhimisho ya miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Akizungumza na waumini hao Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja Rajab Yussuf Mkasaba, amesema kufanyika kwa dua hiyo ni moja ya ibada itakayosaidia kuwengeza nuru na mshikamano katika kuenzi na kuudumisha muungano.

 

Amesema nchi mbalimbali ziliungana na kushindwa kufikia malengo hivyo kuendelea kwa muungano ni moja ya jitihada zinazoendelea kufanywa na viongozi wanayoiyongoza nchi katika kudumisha muungano huo.

 

Hivyo alitumia fursa hiyo kuwataka wananchi kuendelea kushirikiana katika mambo mema na kukatazana maovu ili nchi izidi kupiga hatua kimaendeleo.

 

Wakiongoza dua hiyo ya pamoja  Kadhi wa Wilaya ya Kusini Unguja Abdul azizi Salehe Juma na viongozi wa Kanisa la Katoliki na Kanisa la Anglikana waliomba dua kwa Mwenyezi Mungu kuendelea kuutia nguvu muungano sambamba  na 

kuwaomba waumini kuzidi kuendelea kuwaombea dua waasisi wa muungano na viongozi waliopo madarakani ili wazidi kuuenzi muungano kwa faida ya vizazi vya badae.