Na mwandishi wetu Maulid Khamis Pemba.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Muungano Mh. Hamad Hassan Chande,
amesema yuko tayari kutoa ushirikiano katika vituo vya afya katika kuhakikisha
jamii inapatiwa huduma bora kulingana na utaalamu ikiwa ni pamoja na
kuhakikisha upatikanaji wa vifaa vya tiba.
Mh. Chande ameyasema hayo, huko katika Hospitali ya
Wete wakati alipokuwa akizungumza na madaktari wa vitengo tofauti vya Hospital
hiyo, ambapo amesema tayari ameshaomba ufadhili ambao utasaidia upatikanaji wa
vifaa vya matibabu kwa watoto njiti pamoja na vipimo vyengine kwendana na
wakati.
Nao baadhi ya Madaktari wa Hospitali hiyo wametoa shukurani zao
kwa Mbunge huyo,kwa kuwa na moyo wa kuunga mkono upatikanaji wa huduma bora kwa
watoa huduma pamoja na jamii.
0 Maoni