NA MAULID KHAMIS, PEMBA.
Wakulima wa Mwani shehiya ya kukuu ,Wilaya ya Mkoani wamepatiwa
mafunzo ya kuchakata Mwani, ili kuongeza thamani ya zao hilo kuweza kukidhi
soko la ndani na nje ya Nchi.
Akitoa mafunzo hayo, Afisa kutoka kitengo cha mwani Pemba, Hidaya
Khamis Hamad, amewataka wakulima hao kuyatumia vyema mafunzo wanayopatiwa kwa
lengo la kuongeza thamani utakao changia kukuza pato la mtu moja mmoja na Taifa
kwa ujumla.
Afisa ukaguzi na udhibidi ubora wa bidhaa kutoka taasisi
ya viwango Zanzibar, Hamad Juma Khatib, amewataka wahitimu wa mafunzo hayo
kutengeneza bidhaa zenye ubora na kuhakikisha zinapata usajili kutoka katika
Taasisi ya ZFDA.
Kwa upande wao washiriki
wa mafunzo hayo wameishukuru Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi kwakuwapatia
mafunzo hayo yenye lengo la kuongeza thamani ya zao la mwani.
Mafunzi yaliyotolewa katika hafla hiyo ni utengenezaji wa Sabuni
na mafuta kutumia Mwani unaozalishwa kwa wingi na wakulima hao.
0 Maoni