Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, inampango wa
kununua vitabu vyote kwa ajili ya kusomea wanafunzi wa Primar na sekondari ili
kuondosha changamoto ya upatikanaji wa vitabu pamoja na kuongeza kiwango cha
ufaulu kwa wanafunzi.
Katibu mkuu wa wizara ya elimu Zanzibar Ali Khamis Juma amesema
hayo, katika maadhimisho ya wiki ya maonesho ya vitabu yaliyoandaliwa na Chuo
kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) yaliyowashirikisha wanafunzi wa Skuli ya
Jumbi, halfa iliyofanyika katika ukumbi wa chuo hicho Tunguu na kusema
kuwa mpango huo unatarajiwa kukamilika mwakani.
Amesema hivi sasa mchakato umeshaanza na
wameshafanya mazungumzo na katibu mkuu wa Wizara ya Elimu Tanzania bara ili
kuona watoto wao wanasoma kila mtoto na kitabu chake.
Katibu Ali amefahamisha kuwa hatua hiyo imekuja kufuatia kikao
kilichofanyika na walimu na kueleza changamoto zinazowakabili ikiwemo upungufu
wa vitabu ambapo huko nyuma walikuwa wananunua na kuharimu fedha nyingi.
Aidha amesema wizara yao imeweka utaratibu mpya wa kuwa na
maktaba za nje ya wizara ambapo imeshajenga maktaba moja iliyopo Dunga wilaya
ya kati Unguja na timeharimu shilingi milioni 46 hadi kumalizika kwake.
Nae, Makamo Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) Professa,
Mohammed Makame Haji, amesema, serikali kupitia wizara ya elimu imekuwa ikitoa
mchango kwa wanaotumia vitabu na wanaosoma vitabu.
Mapema Katibu wa Jumuiya ya waandishi wa vitabu Zanzibar, Ali
Mwalim Rashid, alisema, jumuiya yao wapo tayari kuwa mstari wa mbele jatika
kuhakikisha wanaandika vitabu mbalimbali ili kuona vinasomwa katika skuli
mbalimbali na kwenye maktaba zilizopo ndani na nje ya nchi.
0 Maoni