Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Juma S. Mkomi
amesema ushirikiano kati ya Wizara za Kisekta ni nyenzo muhimu katika
kuhakikisha shoroba za wanyamapori haziendelei kuharibiwa
Ametoa kauli hiyo leo tarehe 8 Oktoba, 2022 wakati allipokuwa akizungumza kwenye kikao kazi cha Wataalamu waliokutana Jijini Arusha kwa lengo la kujenga uelewa wa pamoja na kujadili utekelezaji wa Mpango Kazi wa Kuongoa Shoroba za Wanyamapori
‘’Jukumu la ulinzi wa shoroba za wanyamapori ni letu sote kwa maana ya Wizara zetu za kisekta ambazo zinagusa masuala ya Uhifadhi zikiwemo Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Ujenzi na Uchukuzi, Maji, Mazingira na nyinginezo ’’ amesema Naibu Katibu Mkuu, Mkomi
Amefafanua kuwa kikao kazi hicho cha Watalaam ni moja ya hatua muhimu itakayosaidia Wizara zinazohusika na uanzishwaji na usajili wa vijiji, ujenzi wa miundombinu, shughuli za kilimo pamoja ufugaji kuwa na uelewa wa pamoja katika kutekeleza mpango kazi wa kuongoa shoroba hapa nchini.
‘Kikao kazi hiki ni muhimu kwa kuwa kimewaleta wadau kutoka katika sekta mbalimbali mtambuka ambazo zina mchango wa moja kwa moja katika kuhakikisha shoroba za wanyamapori zinalindwa na kuhifadhiwa ‘ amesisitiza Mkomi.
Awali, Mkurugenzi wa Wanyamapori, Dkt.Maurus Msuha amesema kuwa jitihada za makusudi za kulinda shoroba zitasaidia kupunguza migongano iliyopo kati ya binadamu na wanyamapori hususani tembo.
0 Maoni