Na mwandishi wetu

Wananchi wametakiwa kuunga mkono jitihada zinazochukuliwa na serikali ili katika kuleta maendeleo ili kuweza kufikai malengo iliyojiwekea.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar  Hemed Suleiman Abdulla ametoa wito huo alipojumuika na Waumini katika swala ya Ijumaa katika Masjid Jamii Taqwa  Dunga Skuli Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.

 Amesema ni wajibu wa kila mwananchi kuunga mkono jitihada zinzochukuliwa na serikali kwa wananchi wake ili kuwaondolea usumbufu wa upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii.

Mhe. Hemed amewataka wananchi kutosita kutoa taarifa pale wanapoona kuna uharibifu wowote wa miundombinu na uvunjifu wa amani katika maeneo yao ili serikali iweze kuchukua hatua za kisheria kwa maslahi ya wazanzibari.

Aidha Alhajj Hemed amewataka waumini na wananchi kuwaenzi watu wenye mahitaji maalum wakiwemo wajane,walemavu na mayatima ili kuwawekwa sawa na binadamu wengine katika kupata mahitaji na mapenzi miongoni mwao.

Amesema kuwa kila mmoja kwa nafasi yake  kuhakikisha anatoa ushirikano wa hali ya juu kwa makundi hayo maalum ili kuondosha changamoto ambazo huwakumba watu wa aina hio ikiwemo suala la udhalilishaji.

Kwa upande wake Imamu wa Msikiti huo  Sheh. IS-HAKA VUAI KIDAWA  amewataka Waumini na Viongozi wanaosimamia mirathi kwa mayatima na wajane kusimamia haki zao kama dini inavyosema ili kupata fadhila hapa duniani na kesho ahera.

 

Amesema ni wajibu kwa kila muumini na kiongozi wa familia kuwa na malezi mazuri kwa mayatima na wajane ili kuweza kupata fadhila za Allah S.W na kuwataka wazanzibari kurudisha malezi ya zamani kwa vijana ili kupata jamii iliyo bora.