Na mwandishi wetu
Masheha wa Wilaya ya
Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, wameshauriwa kuihamasisha jamii
kujikita Zaidi katika ukulima wa kilimo cha miwa
ili kuongeza kipato na kukidhi uzalishaji wa mali ghafi ya
kiwanda cha Sukari Mahonda
Mkuu wa Wilaya hiyo
Marina Joel Thomas, amesema hayo alipokuwa katika kikao na Masheha wa Wilaya
hiyo na Uongozi wa kiwanda cha sukari Mahonda waliofika katika ofisi ya Baraza
la Mji Kati Dunga kwa lengo la kuwashajihisha wananchi kulima kilimo hicho.
Amesema licha ya
juhudi mbali mbali zinazoendelea kuchukuliwa na uongozi wa
kiwanda hicho kuzalisha zao hilo lakini bado wanakabiliwa na
uhaba wa maeneo ya uzalishaji wa zao hilo hivyo kupatikana
kwa maeneo mengine kutasaidia kuongezeka kasi ya uzalishaji wa sukari kwa
wingi hali itayochochea ukuwaji wa uchumi wa nchi na wananchi
kwa ujumla.
Nao baadhi ya viongozi
wanaosimamia uendeshaji wa kiwanada hicho Bwana Mohamed Said
Dimwa na Bwana Hindi Said Mohammed wamesema ikiwa masheha watahamasisha ipasavyo
wananchi katika maeneo yao itasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza uzalishaji wa
zao hilo na kupata ajira kwenye sekta hiyo..
Nao baadhi ya masheha
wamepongeza hatua ya uongozi wa kiwanda hicho na kuahidi kuihamasisha jamii
juu ya suala hilo ambalo litawaletea manufaa katika maisha yao ya kila
siku.
MAJINA YA MASHEHA HAO : ND:Tatu Sheria Shaban Sheha wa Shehia ya Cheju Zawiani na Sheha waShehia ya Jumbi Muhidini Haji Machano waliahidi.
0 Maoni