Na Mwandishi nwetu

Makamo wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Adbullah anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika Michuano ya Green Cup hatua ya Nusu Fainal inayotarajiwa kufanyika siku ya Jumapili ya Desember 5, 2021, katika Uwanja wa amani

Kasmir Haji ambae ni  katibu  msaidizi Mkuu Idara ya Uhamasishaji na Chipkizi Tanzania  ambae anaefanyia kazi zake Zanzibar, ametoa taarifa hiyo mbele ya waandishi wa habari katika kikao kilichofanyika hii leo Dec 2, 2021, kwenye ukumbi wa Ofisi za umoja wa Vijana (UVCCM) Zanzibar, zilizoko Gymkana Kikwajuni Mkoa wa Mjini Magharib.

Amesema Hatua hiyo ya Nusu fainali itakayohudhuriwa na Mhe Hemed itakuwa na michezo Miwili ambayo yote itachezwa siku moja, ambapo kutakuwa na Mchezo wa Mapema saa nane utakaowakutanisha  Mkoa wa Pwani na Tabora na Mchezo utakaofuatia utachezwa saa kumi kwa kuwakutanisha Wenyeji Magharibi wawakilishi pekee wa Zanzibar ambao watacheza na Mkoa wa Morogoro

Katibu Kashmiri amesema Mkoa wa Morogoro,Tabora, Pwani na Mkoa wa Mgharibi ndio ambao wamefanikiwa kupita katika hatua hiyo Nusu fainal na Maandalizi kuelekea mchezo huo tayari yameshakamilika.

‘‘Maandalizi yote yamekamilika na mhezo wa saa nane tutakua nae Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Tanzania ndie atakaekua Mgeni Rasmi na mchezo wa saa kumi tutakua na kiongozi Mkubwa ambae ni makamo wa Pili wa Rais Zanzibar na Jumamosi tunatarajia kupokea timu zote zinazokuja kutokea Tanzania Bara’’.

Kwaupande Mwengine Katibu Kasmiri amesema kutazama michezo hiyo ni bure na hakuta kuwa na kiingilio chochote hivyo, ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwawingi kushuhudia burudani mabli mbali siku hiyo ikiwemo Benin na  n.k

Wa kwanza kushoto ni Ngd. Kasmir Haji ambae ni  katibu  msaidizi Mkuu Idara ya Uhamasishaji na Chipkizi Tanzania,  anaefanyia kazi zake Zanzibar katika mkutano na waandishi wa habari na wa kwanza kutokea kulia ni Bi Nahla Abduli Hasan katibu wa Hamasa Mkoa wa Mjini Kichama.
Wa kwanza kushoto ni Ngd. Jemsi Michael Chirwa ambae ni Katibu Oganaizeshen wa Umoja wa Vijana Ofisi ya Zanzibar, aliekaa kati kati ni Kasmir Haji ambae ni  katibu  msaidizi Mkuu Idara ya Uhamasishaji na Chipkizi Tanzania,  anaefanyia kazi zake Zanzibar katika mkutano na waandishi wa habari na wa kwanza kutokea kulia ni Bi Nahla Abduli Hasan katibu wa Hamasa Mkoa wa Mjini Kichama.