Na Suleiman Mohamed
Wakala wa udhibiti
Chakula,Dawa na Vipodozi Zanzibar (ZFDA)
wamesema wamejiridhisha kupitia miongozo ya Shirika la Afya Duniani kua Chanjo za UVICO 19 zilizothibitishwa na
Serikali kutumika Zanzibar ni salama na zina ubora unaokubalika.
Hayo yameelezwa
na ----Bi Hidaya Juma Hamad, Mfamasia kutoka Wakala Wa Chakula, Dawa na
Vipodozi, wakati wa Mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa
Habari juu ya utoaji elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa chanjo hiyo yaliyofanyika
katika Hotel ya Golden Tulip Bububu Wilaya ya Magharibi A, Mkoa wa Mjini
Magharibi Unguja.
Amesema Wakala wa Chakula Zanzibar kabla ya
kuingia kwa Chanjo hapa Nchini walitumia kila Njia kuhakikisha wanajiridhisha
Ubora na usalama wa Chanjo hizo kama ilivyo kwa Chanjo nyengine kuhakikisha
zinakua salama na ubora unaokubalika
‘‘tulishirikiana
na Shirika la Afya Duniani katika
kutumia Miongozi katika kujilijiridhisha kua inakua na Ubora na Usalama pia hua
tunafanya mawasiliano na wenzetu mara kwa mara kwa pale ambapo tunapohisi iko
haya ya kujiridhisha zaidi na sio kwa chanjo hii ya UVICO 19 tu hata chanjo
nyengine zinazoingia hapa nchini hua tunajiridhisha kabla ya matumizi’’
Kwa upande wake
Mratibu wa Kitengo cha Elimu ya Afya, kutoka Wizara ya Afya, Wazee, Ustawi wa
Jamii Wanawake na Watoto Zanzibar Bi Halima Khamis amesema Serikali inatoa chanjo hizo
bure kwa lengo la kuwakinga wananchi wake na UVICO 19 hivyo wananchi waepukane
na dhana potofu na badala yake wajitokeze kwa wingi kupata Chanjo hiyo.
Amesema katika
kuhakikisha hudma za Chanjo zinawafikiwa wananchi wengi Serikali imeongeza
Vituo vya kutolea huduma katika kila Wilaya na Mikoa kwa Unguja na Pemba ambpo
kuna jumla ya Vituo vipatavyo Thelathini na Nane (38).
Hadi sasa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Tayari imeidhinisha Jumla ya Chanjo sita kutumika hapa Zanzibar ikiwemo Sputnilc Light, Sinovac, Moderna, Pfizer,sinophac, na Johnson & Johson.




0 Maoni