Na mwandishi wetu
Chama Cha Democrasia Makini
ofisi ya Zanzibar Kuiunga mkono asilimia Mia Moja (100) hutuba ya Raisi wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi alioitoa
hapo juzi katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Mkoa wa Mjini Mgharib.
Katika Taarifa hiyo
aliyohutubia kwa vyombo vya Habari akiwa Ofisini kwakwe Taveta Wilaya ya Mjini,
Katibu katibu Mkuu wa Chama hicho Ameir Hassan Ameir amesema hutuba hiyo ya Dr
Mwinyi imeleta matumaini makubwa kwa wananchi wa Zanzibar.
Amesema hotuba hiyo imeainisha
namna Serikali ya Dr Mwinyi watakavyoshuhulika na Changamoto zinazowakabili
wananchi hasa katika sekta ya Elimu, Afya, Maji, Umeme na kuwawezesha
wajasiriamali maeneo ambayo naamini yakifanyiwa kazi vizuri yatachangia pakubwa
kuinua uchumi wanchi.
Aidha amewaomba
wasaidizi wake ikiwemo Mawaziri, Makatibu na wataalum wa idara kuhakikisha
wanafanya kazin kwa uaminifu na kuhakikisha wanamsaidia Mh Rais kutimiza azma
yake kwaWananchi wa Zanzibar
Katika hatua nyengine
Amer Hasan Amer amemuomba Mh Rais kuhakikisha anasimamia vema Fedha zilizotolewa na IMF ili zitumike ipasavyo
katika kusaidia Changamoto za wananchi.
0 Maoni