Na mwandishi wetu
MAKAMU wa Kwanza wa
Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar ipo tayari kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa
Linaloshughulikia Maendeleo ya Mtoto UNISEF, kuifanyia mapitio sera ya
Maendeleo ya Mtoto Zanzibar, ili iweze kwenda sabamba na mweleko wa mahiji ya serikali yaliyopo sasa.
Mhe. Othman ameyasema
hayo leo Ofisini kwake Migombani mjini Zanzibar alipozungumza na Mwakilishi
Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Maendeleo ya Mtoto
Duniani Bibi Laxmi Bhawani.
Bibi Laxmi alifika Ofisini kwa Mhe. Othman kwa mazungumzo rasmi
yaliyohusu ushirikiano kwa masuala mbali
mbali na Zanzibar, ikiwemo maendeleo ya mtoto, lishe pamoja na suala la
utunzaji na hifadhi Mazingira ya Zanzibar.
Aidha amesema kwamba
kutokana na mambo mbali mbali yanayojitokeza katika utekelezaji wa sera hiyo, hivi sasa inahitaji kufanyiwa
mapitio sambamba na kusaidia mpango wa
kuimarisha liche ya mtoto katika kujenga mustakbali bora wa maendeleo ya mtoto
wa Zanzibar.
Amefahamisha kwamba
shirika hilo kwa muda mrefu limekuwa na mchango mkubwa kuisaidia Zanzibar katika masuala mbali mbali
ya maendeleo ya mtoto hasa wenye mahitaji maalum na lishe ambapo masuala hayo yamepewa umuhimu mkubwa katika kujenga maendeleo ya mtoto Zanzibar.
Mhe. Othman amesema
katika majadiliano hayo pamoja na mambo mengine pia wamekubaliana
kushirikiana katika kustawishi mahitaji
mbali mbali ya watoto wenye mahitaji maalum Zanzibar hasa katika maeneo ambayo
yanayonekana kuwa na matatizo zaidi katika ustawi na maendeleo ya mtoto.
Akizungumzia suala la
utunzaji wa Mazingira, amesema kwamba
wamekubalia kutumia mbinu za pamoja za utunzaji na uhifadhi wa mazingira
ikiwemo suala la taka ii yawe na faida kwa maendeleo ya mtoto na taifa kwa
kujmla.
Amesema watoto wenye
mahitaji maalum hasa katika maeneo kama vile ya Micheweni ambayo
yanaonekana yapo nyuma kwa kuwepo matatizo mengi zaidi yanayoathiri maendeleo
ya mtoto katika ukuaji na uimarishaji wa mfumo wa lishe yatapewa kipaumbele.
Hata hivyo, amesema
katika jitihada hizo za pamoja pia mashirikiano yataelekezwa katika utoaji wa
elimu zinaohusu mazingira, maendeleo ya
mtoto pamoja na liche bora ili kuwajenga watoto kukua vyema kimwili na kiakili
kwa maendeleo ya taifa.
Kwa upande wake
Mwakilishi hyo makaazi wa Unisef Laxmi Bhawani amesema kwamba Shirika la
UNISEF lipo tayari kushirikiana na
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika
kusaidia mambo mbali mbali kwa maendeleo ya mtoto na Zanzibar kwa jumla.
Amesesema pia shirika
lake litaimarisha mashirikiano ya wadau na jamii katika kukuuza upatikanaji wa
lishe bora kwa watoto sambamba na kutoa elimu kujenga mwamko wa jamii kwa
matumizi sahihi ya chakula chenye kujenga liche bora kwa watoto.
Amesema kwamba
UNISEF jitiuhada za pamoja kati ya
UNISEFU na Zanzibar yatasaidia kujenga
uelewa zaidi kwa jamii na kwamba masuala hayo yamepewa umuhimu wa kipekee
katika kusaidiana na Serikali ya Zanzibar kuwajengea mustakabali bora watoto .
0 Maoni