RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi na Mkewe Mama Mariam Mwinyi  akiondoa kipazia kuashiria kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hoteli ya Kitalii ya Riu Hotels & Resorts Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja (kushoto ) Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud na Bw.Raul Gantes wakiondoa kiupazia, hafla hiyo imefanyika katika eneo la ujenzi huo Nungwi, ikiwa ni shamrashamra za kutimiza Mwaka mmoja  wa Uongozi wake

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr Hussen Ali Mwinyi amewaagiza Viongozi wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanaweka utaratibu utakaohakikisha bidhaa wanazozalisha wananchi zinauzwa katika Mahotel ya kitalii ndani ya maeneo yao badala ya kuhangaika kutafuta Masoko

Rais Mwinyi ameyasema hayo Novomber 3 wakati akiweka jiwe la Msingi katika Hoteli ya Riu Jambo iliyopo Nungwi, wakati wa Ziara yake katika shamra shamra za kuadhimisha Mwaka mmoja tokea aapishwe kuwa Rais November 2 mwaka Jana (2020)

Amesema ni Vema Miradi mikubwa inayojengwa karibu na Jamii ikiwemo mahotel yakawanufaisha wananchi wanaozungukwa na Miradi hiyo katika kuleta maendeleo kwapamoja.

 Katika hatua nyengine Rais Mwinyi amesema  wawekezaji wa miradi hiyo wanapaswa kushirikiana na Jamii katika kuwasaidia changamoto zinazowakabili ikiwemo changamoto ya elimu, afya, maji na mengineyo kwa kushirikiana na Serikali.

 Rais Mwinyi alipata nafasi ya kuweka jiwe la msingi katika hoteli nyengine ya Emerald Zanzibar Resort and SPA iliyopo matemwe ambapo baada ya kuweka jiwe la msingi alipata nafasi ya kuwasalimia  wananchi  wa Matemwe Mbuyuni huku akiwataka  kuendelea kuthamini  sekta ya utalii kwakua  ndio sekta inayochangia  kukua kwa pato la Taifa.

 Nao wawekezaji wa Hoteli ya Riu Jambo ambapo ujenzi wake ulianza Januarimwaka huu 2021 waliwahakikishia wavuvi wa maeneo hayo kwamba mradi wa Hoteli yao utakapokuwa tayari kufanya kazi samaki wote watakaovuliwa katika eneo hilo watanunuliwa na hoteli yao ili kuhakikisha wavuvi hao wanapata soko la uhakika pamoja na kuwajengea soko na miradi mengine ya jamii.

 Kwa mujibu  wa maelezo ya uongozi wa Hoteli hiyo, mradi huo unatarajiwa ujenzi wake kumaliza mnamo Septemba mwakani 2022, na utaajiri  wafanyakazi 400 huku hoteli hiyo itakuwa na vyumba 468 ambapo ujenzi wake utagharibu zaidi ya Dola za Kimarekani milioni 70.

 Kwa upande wa Hoteli ya Emerald Zanzibar Resort and SPA ambayo ujenzi wake ulianza Novemba mwaka jana 2020 unatarajiwa kumaliza mwakani 2022, mradi ambao kwa akuanzia utakuwa na vyumba 250 na hadi kumaliza katika awamu zijazoitakwua na vyumba 1000.