Na Mwandishi wetu

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kaskazini Pemba Asya Sharif Omari amesema Raisi wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Samia Suluh Hasan ni Kiongozi Shupavu na  aliejitolea kupigania maendeleo ya Watanzania kwa kasi kubwa

 

Mbunge Asya ameyasema hayo wakati akizungumza na mwandishi wetu  kwa njia ya simu akiwa  Dodoma kwa lengo la kupata tathimni yake kuhusu safari ya Rais Samia Nchini Misri,  ambapo amesema Wanawake katika Nchi hii na Bara zima la Afrika wanapaswa kujivunia kutokana na kuwakilishwa Vizuri na Uongozo wa Rais Samia.

 

‘‘unajua wako ambao hawakuamini kama mwanamke anaweza kua Rais na akafanya vizuri kiasi hki anachofanya Samia yaani anatuwakilisha vizuri sana na sasa heshima ya mwanamke imeendelea kuheshimiwa kutokana na kazi nzuri anayoifanya Mhe Rais Samia’’

 

Amesema ni vema watu wakaelewa Safari ambazo Mhe Samia amekua akizifanya Nje ya Nchi zina tija kubwa kwa Maslah ya Tanzania ikiwemo Nyanja za Utalii, mioundombinu,uwekezaji na masuala mengine ya kulimo na Afya

 

‘ ‘Sikia mtangazaji Rais Jana tu amerejea kutoka Misri na zafari yake haikua na usiri kila kitu kilikua wazi, angalia ametembelea makampuni Makubwa ikiwemo wale wanaojenga Bwawa la umeme, vilevile amefanya kikao na wafanyabiashara wa Misri katika kuhakikisha fursa za uwekezaji zinatangazwa hapa nchini’’

  

Mbunge Amesema Raisi Samia katika safari yake Nchini Misri ameshuhudia utiaji saini mkataba mmoja na hati saba za makubaliano kati ya Tanzania na Misri ambazo hizo ameeleza kama hatua za kiamaendelea Serikali iliyozifikia na suala la kukuza Diplomasia.