Na Mwandishi wetu
Vingozi wa Shehia pamoja
na wadau wa maendeleo wa Wilaya ya Micheweni wametakiawa kuongeza nguvu
katika kuandaa mikakati imara itakayosaidia mradi wa kuwarejesha watoto
watoro mashuleni unafanikiwa kikamilifu.
Mkuu wa wilaya ya
micheweni, Mh. Mgeni Khatib Yahya ameyasema hayo, katika ukumbi wa Halimashauri
ya Wilaya ya Micheweni Kaskazini Pemba, wakati akizungunza na viongozi wa
Shehiya za Wilaya hiyo katika kikao cha Mikakati chenye lengo la kuwarejesha
watoro Shuleni
Amesema iwapo viongozi wa shehia
watakuwa na ushirikiano baina yao na watu wanaowaongoza katika maeneo yao,
jamii itanufaika vyema katika suala la
elimu.
Akijibu hoja za wachangiaji
katika mkutano huo, Afisa mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba, Nd.
Mohamed Nassor Salim, amesema kwa upande wao Wizara ya Elimu
iko tayari kuunga mkono jitihada za wadau katika kukamilisha malengo ya mradi huo
kwa kutoa elimu kwa jamii, ili waweze kushiriki kwa faida ya vizazi
Vijavyo.
Akitoa takwimu Afisa Kisomo
Idara ya Elimu Mbadala Pemba, Nd. Haji Juma amesema, lengo kuu la
elimu mbadala nikuwarejesha wale wote ambao wameacha Shule
na wale ambao hawakusoma.
Nao baadhi ya
washiriki hao Sheha wa Shehiya ya Shumba Mjini Rahla Ramadhan na Sharifa Suleiman
Mwalimu wa Darasa la Watoto watoro, kutoka Skuli ya Tumbe Msingi, wamesema
tayari wameanza utekelezaji wa mikakati katika Shehiya zao kwani
wanaelewa vyema umuhimu wa elimu kwa jamii hasa vijana.




0 Maoni