Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa ndugu Lela Mohammedi Ngozi, wakati akizungumza na wanahabari katika kutoa kauli ya chama cha Mapinduzi kwa Uongozi wa Mwaka Mmoja Madarakani  Rais Hussen Ali Mwinyi

 Na Suleiman Kidudu

Chama mapinduzi  CCM Zanzibar  kimesema kinaridhishwa na Kasi ya utendaji kazi wa  Raisi wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dokta Hussein Ali Mwinyi  Ndani ya mwaka Mmoja wa uongozi wake .

 Hayo yameelezwa na mjumbe wa halmashauri kuu ya ccm Taifa ndugu Lela Mohammedi Ngozi wakati Akizungumza na waandishi wa habari Kwa niaba ya Naibu katibu mkuu wa Ccm Zanzibar Abdlalha Juma Sadala (Mabodi)  katika  ukumbi wa Afisi Kuu ya Chama hicho kisiwandui mjini Unguja .

 Ndugu Leila emesema ndani ya mwaka Mmoja tayari ameonesha mwanga wa mafanikio katika sekta mbali mbali  zinazolenga kukuza uchumi wa Nchi pamoja na kukuza uchumi wa Mzanzibar mmoja mmoja .

 Ndugu Lela amefahamisha kuwa Rais Mwinyi Amedhamiria kuleta mabadiliko ya haraka ndani ya Zanzibar na kuahidi chama kuendelea kumuunga mkono katika harakati zote za Maendeleo .

 Aidha ndugu Lela ametaja baadhi ya maeneo ambayo Raisi Mwinyi amefanya kazi ikiwemo kupambana na wabadhilifu wa Mali za umma  ,mapandano dhidi ya udhalilishaji pamoja na kuendeleza mapambano dhidi ya dawa za kulevya kwani  hayo Yote yamekuwa yakisababisha ukuaji mdogo wa uchumi wa Taifa .

 Katika hatua nyenginea  chama Cha mapundizi kimempongeza Dokta Mwinyi Kwa Kwa kufika hatua nzuri za ujenzi wa Miradi mikubwa ya kimaendeleo ikiwemo Ujenzi wa Bandari ya Manga Pwani pamoja na Ujenzi wa Bandari ya Mpiga duri 

 Katika hatua nyengine Chama hicho cha Mapinduzi kimempongeza Rais Mwinyi kwakuongeza ukaribu zaid na Viongozi wa Dini mbali mbali kutokana na umuhimu wao katika Jamii na Mchango Mkubwa wanaoendelea kuutoa katika Jamii.

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa ndugu Lela Mohammedi Ngozi (aliekaa kati kati) kushoto ni Mjumbe wa Halmashauri kuu Taifa ambae Pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Magharibi Kichama Mohamed Rajabu na aliekaa kulia ni Kimtende, Afisa msaidizi katika idara ya Uenezi Zanzibar