Na mwandishi wetu

 Afisa Mdhamini wa Wizara ya uchumi wa buluu na uvuvi Dk. Salim Mohd Hamza amezitaka taasisi husika kusimamia sheria inayosisitiza maeneo ya uhifadhi na kuwalinda samaki mama, Pomboo pamoja na rasilimali nyengine ili kudhibiti uharibifu unaofanywa na binaadamu.

Amesema kwa sasa kumekithiri vitendo vya uharibifu wa rasilimali za bahari unaofanywa na binaadamu  hali inayopelekea kuharibu mazalia ya samaki hivyo iwapo taasisi husika zikasimamia sheria hiyo itasaidia kupunguza vitendo hivyo.

Hivyo ameitaka tume ya sheria kuongeza vifungu vya usimamizi wa samaki wa mapambo na maji baridi ili kuendana na wakati uliopo.

Nae Afisa kutokea tume ya kurekebisha sheria Mohammed Abdurahman Mohammed amesema kazi ya ukusanyaji wa maoni ya sheria  namba 7 ya maendeleo ya uvuvi na uhifadhi wa maeneo ya baharini kwa unguja na pemba imeenda vizuri

Aidha amewataka wananchi mbalimbali ambao hawajatoa michango yao katika vikao vya ukusanyaji wa maoni kutumia njia ya maandishi kwa ajili ya kutoa maoni yao na kupeleka katika idara husika ili kushiriki kwa ajili ya maendeleo ya taifa .

Akifunga  kikao hicho Mkurugenzi wa idara ya maendeleo ya uvuvi na mazao ya baharini Zanzibar Dk Salum Soud Hammed ameahidi kuzipatia ufumbuzi baadhi ya changamoto ikiwemo changamoto za leseni kwa wavuvi wa zanzibar na tanzania bara ili kuonesha kifungu kitachosimamia uvuvi bila ya uonevu kwa pande zote mbili.

Taasisi zilizoshiriki kikao hicho ni tume ya kurekebisha sheria,idara ya maendeleo ya uvuvi na mazao baharini na vyombo vya usalama wa raia pamoja na mamlaka za serikali ya mapinduzi ya zanzibar.