Na Mwandishi wetu Kaije Salum
Walimu wa mpira wa miguu Visiwani Zanzibar
wametakiwa kubadilika kulingana na mabadiliko yanayojitokeza katika soka ili
kwenda sambamba na Mabadiliko ya sheria
Kauli hiyo imetolewa na mkufunzi wa makocha Muhamed
Tajdin katika Uwanja wa Gombani Wilaya
ya Chakechake Kisiwani Pemba wakati
akiongoza mafunzao kwa wanafunzi wapya wa fani hiyo.
Amesema masomo hayo yatakuwa ya siku kumi na
yatahusisha sehemu nne kwa makocha hao wapya ambazo ni kujifunza Nadharia ya
mpira, mpira kwa vitendo, tiba na sheria.
Ameeleza sasa niwakati muafaka wa kujenga mahusiano
kati ya ZFF na TFF kwa ajili ya kuendeleza na kukuza soka la Tanzania
ambalo limeonesha mwanga wa kupiga hatua.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa ufundi kutoka ZFF
Muhamed Said Abdalla alisema kazi ya ukocha ni ngumu na inahitaji kuwa na
elimu.
“Awali kulikuwa hakuna vigezo vinavyo hitajika
kufundisha lakini sasa wakati umefika kufanya kazi kwa kutumia vielelezo vya
kielimu”alisema mkurugenzi huyo.




0 Maoni