RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwahutubia Wananchi wa Wilaya ya Chakechake Pemba katika ufunguzi wa jengo jipya la Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) lilioko katika eneo la Gombani Pemba, hafla hiyo ya ufunguzi imefanyika katika viwanja vya jengo hilo 

Na mwandishi wetu

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa ujenzi wa jengo jipya la Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Pemba ni utekelezaji wa dhamira ya Serikali ya kuimarisha mazingira mazuri ya kufanyia kazi kwa watumishi wa umma ili kuongeza ufanisi katika utendaji na utoaji huduma kwa wananchi.

Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo katika uzinduzi wa Jengo jipya la Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB), huko Gombani, Wilaya ya Chake Chake,  Mkoa wa Kusini Kisiwani Pemba.

Katika hotuba yake Rais Dk. Mwinyi amesema kazi kubwa imefanywa na Serikali ya Awamu ya Saba katika kuimarisha mazingira ya kufanyia kazi kisiwani Pemba ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Ofisi za Serikali zilizopo Gombani, Jengo jipya la ZSSF pamoja na majengo mengine mengi ambapo kila Wizara ina ofisi ya kisasa kisiwani Pemba.

Amesema kuwa majengo ya kisasa yaliyojengwa sio tu kwamba yana mchango mkubwa katika mazingira ya kufanyia kazi bali pia yanaongeza taswira ya mji pamoja na kuufanya mji uwe wa kupendeza.

Ameongeza kuwa ujenzi wa ofisi za kisasa ni hatua muhimu katika utekelezaji wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Nane ya kukifanya kisiwa cha Pemba kuwa  ni eneo maalum la kimkakati la uwekezaji sambamba na kuhakikisha kwamba huduma na mahitaji muhimu kwa wananchi na wawekezaji yanayopatikana Unguja pia, yapatikane kisiwani Pemba.

 Ameeleza umuhimu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Bodi ya Mapato (ZRB) kufanya kazi kwa pamoja, na kusema kwamba kuwepo kutoa huduma Pemba kutasaidia wananchi.

 Nae Waziri wa Fedha  na Mipango Jamali Kassim Ali alisema kuwa jengo hilo lina mambo yote muhimu ya kufanyia kazi na kuweza kuwarahishia kuweza kutoa huduma bora kwa wateja hasa wale walipa kodi.

 Mapema Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Dk. Juma Maliki Akil, alisema kuwa jengo  hilo linachochea kuleta utulivu wa kufanyia kazi na kutoa huduma bora kwa wananchi.

 Pia, jengo hilo kutokana na miundombinu yake kutakuwa na usalama wa kutosha na ulinzi pamoja na utunzaji bora wa kumbukumbu wa nyaraka kutokana na mfumo mliojengwa wa tehama katika jengo hilo.

Pia, litakuwa na kitengo cha dharura, na kuwa na huduma za kuaminika hasa huduma za umeme ambapo litakuwa na umeme muda wote hata pale huduma hiyo ikikosekana.

 Jengo hilo lina ghorofa nne, ghala, na sehemu nyenginezo ambapo kuanzia ghorofa ya kwanza hadi ya nne kuna vyumba kwa ajili ya wafanyakazi mbali mbali , pamoja na kuwepo kumbi mbali mbali.

Sambamba na hayo, Katibu Mkuu huyo alisema kuwa mkataba wa ujenzi wa jengo hilo ulitiwa saini mwezi Disemba 2019 kati ya ZRB na Mkandarasi ‘Advent Construction Limited’ ambaye ni kutoka Dar-es-Salaam .na kukamilika rasmi mwezi Mei mwaka 2021 kwa gharama za TZS Bilioni 10.6.

 

WAFANYAKAZI wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa jengo jipya la ZRB Gombani Wilaya ya Chakechake Pemba
wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Mhe.Jamal Kassim Ali akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa jengo la Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Gombani Wilaya ya Chakechake Pemba, kabla ya kumkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi. 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi na (kulia kwa Rais)Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi na (kushoto kwa Rais) Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi.Zena Ahmed Said, wakimsikiliza Kamishna Mkuu wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Bw. Salum Yussuf Ali, akitowa maelezo wakati wa kutembelea jengo hilo baada ya kufunguliwa rasmin
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi na (kulia kwa Rais) Mama Mariam Mwinyi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya ZRB Bw. Saleh Sadoq na (kushoto kwa Rais) Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said, wakitembelea jengo hilo la ZRB baada ya kulifungua leo rasmin.(
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikata utepe kulifungua jengo jipya la Bodi ya Mapato Zanzibar.(ZRB) lilioko katika eneo la Gombani Wilaya ya Chakechake Pemba na (kulia kwa Rais) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya (ZRB) Bw.Saleh Sadiq na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Mhe.Jamal Kassim Ali na (kushoto kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe.Mattar Zahor Masoud.(