Serikali ya Omani
inatarajia kutoa msaada wa kifaa cha kuangalia Mwezi mwandamo kwa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar ili kuiwezesha ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar kutumia teknolojia katika
shuhuli za utafutaji wa Mwezi kama ilivyo katika mataifa mengine yaliyoendelea.
Kifaa hicho
kinatarajiwa kufika mwaka huu kabla ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Hayo yamesemwa
na Balozi Mdogo wa Oman, Said Salum Al-sinawi katika Ofisi ya Mufti wa Zanzibar
iliyopo Mazinizi Mkoa wa Mjini Magharib alipofika ofisini hapo kwaajili ya kujitambulisha kufuatia Balozi aliokuwepo
awali kumaliza mda wake.
Amesema Zanzibar
na Serikali ya Omani ni watu wenye udugu wa damu kwa mda mrefu, hivyo ipo haja
ya kuisaidia katika kila nyanja ya maendeleo.
“Mimi naelewa
kuwa Zanzibar na Oman ni ndugu wa damu tutakuwa pamoja ili kuendeleza udugu
wetu” alisema Balozi huyo.
Amesema anacho
kifanya hivi sasa ni kuangalia maombi yote yaliyofika mezani katika ubalozi huo
ambayo yamepangwa kutekelezwa na Balozi aliepita na kuyapa umuhimu na kuyafanikisha
kwani hilo ndio jukumu lake .
“Nimeona maombi
yenu mara tu kufika Ofisini ni jambo jema nitashughulikia hilo ni masuala
muhimu kuweza kutekeleza”, aliongeza kusema balozi huyo.
Amesema ameyaona
maombi yao yapo mezani ikiwemo maombi ya uendelezaji wa ujenzi wa Ofisi ya
mufti,kifaa chakuangalizia mwezi na mambo mengine mengi ambayo ni muhimu.
”Nimeona maombi
na nitayafanyia kazi na hichi kifaa chakuangalizia mwezi kitafika kabla ya
Mwezi mtukufu wa Ramadhani”,alisema Balozi Ali Salum.
Nae Mufti wa
Zanzibar sheikh Saleh Omar Kabi, alimshukuru kiongozi huyo kwa ujio wake kufika
ofisini hapo na kusema ujio huo ni kuendeleza udugu wao wa damu ambao Zanzibar
inafaidika sana na Misaada ya Serikali ya Omani ikiwemi ujenzi wa Misikiti,nyumba
za kihistoria,vyuo na maeneo mengine ya kijamii.
Mufti huyo
alisema, Omani iendelee kuisaidia Zanzibar na isiishie hapo kwani misaada yao
imekua ni chachu ya kuendeleza masuala ya dini ya kislamu katika visiwa vya
Zanzibar hivyo ni muhimu sana kuona dini ya kislamu inasimamiwa misingi yake.
Aidha mufti huo
alisema kuwa wao wako tayari kuendelea na kuisimamia ofisi hiyo kwa nia safi
ili kuendeleza uislamu na kusimamia taratibu zake.
SK-News TV
WAFUATILIAJI
Tafuta Habari
Kuhushu SK News
SK News
SK Blog, ni blog ya kijamii inayojihusisha na Utoaji wa taarifa za Kijamii, Habari, Michezo, Siasa, Uchumi, Mahusiano, na Burudani.
0 Maoni