Mbunge wa Viti
Maalum Mkoa wa Kaskazini Pemba Asya Sharif Omari amempongeza Rais wa Jamhuri wa
Muungano wa Tanzania kwa kuhudhuria Mkutano wa Mabadiliko ya Tabia ya Nchi,
uliofanyika jana September
21,Nchini Marekani.
Mhe Asya amesema
kitendo cha Rais Samia kusafiri hadi Nchini Marekani kwaajili ya kuhudhuria
mkutano huo ni jambo jema kwakua Tanzania ni sehemu ya Dunia hivyo
inahitaji kushirikiana na Mataifa Mengine Dunia katika kila Jambo hasa
ukiangalia umuhimu wa Mkutano wenyewe.
‘‘Rais samia
anafanya kazi kubwa sana, tumeona tokea aapishwe amekua akifanya kazi kubwa
ndani na Nje ya nchi , lakini kubwa amekua akizunguka kuangalia namna gani
atashirikiana na mataifa mengine kwaajili ya maendeleo ya Tanzania, kwakweli
anatuwakilisha vizuri na anaionesha Dunia kuwa Wanawake tunaweza’’amesema Mh Asya.
Mhe Asya amesema hayo leo (September 22) akiwa Visiwani Zanzibar wakati wa mazungumzo na mwandishi wetu ambapo amesema safari hizo za Mhe Samia zina umuhimu mkubwa na hasa ukizingatia kipindi hichi cha korona kila taifa linaangalia namna gani ya kusimama kwaajili ya kuboresha uchumi wake uliotetereka kwa Uvico 19.
Katika hatua
nyengine Mhe Asya amesema Rais Samia anafanya kazi kubwa ya kuitangaza Tanzania
Kimataifa hivyo watanzania watarajie kuendelea kuona maendeleo mengine makubwa
ikiwemo kuongezeka kwa wawekezaji na kuimarika kwa diplomasia zaidi katika
kipindi hiki cha uongozi wake.
‘‘unajua ndugu
mwandishi juzi tu tumeshuhudia Rais akirekodi kipindi maalum cha Royal Tour, kile kipindi kitakwenda kuitangaza Tanzania
na sasa tutarajie kuona watalii wengi wakiingia Tanzania na Zanzibar na hata wawekezaji lakini kubwa kuimarika
kwa Diplomasia kati ya mataifa ya Nje na Tanzania’’ amesema Mhe Asya
Rais Samia ni
Miongoni mwa Viongozi wakuu wa Nchi waliohudhuria Ufunguzi wa Mkutano wa 76
uliofanyika Nchini Marekani.
Wakati huo huo, Mheshimiwa Rais Samia leo pia
amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Comoro, Mhe. Azali Asoumani na
Makamu wa Rais wa Sudan Kusini, Mhe. Rebecca Nyandeng Garang. Viongozi hao
wamezungumzia kuimarisha uhusiano na ushirikiano baina ya Tanzania na mataifa
hayo.







0 Maoni