Mkurugenzi wa TAMWA-ZNZ Dkt,Mzuri Issa akieleeza umuhimu wa vyombo vya
habari kuwaunga mkono wanake kushika nafasi za uongozi.Mkurugenzi wa Chama cha Waaandishi wa habari Wanawake TAMWA-ZNZ Dkt,Mzuri Issa amesema katika jitihada za kuwaunga mkono wanawake kushika nafasi mbali mbali za uongozi vyombo vya habari vinawajibu wa kutoa kipao mbele habari zinazowahusu wanawake viongozi na wale wote ambao wanahitaji kupaziwa sauti zao kwa lengo la kuleta mabadiliko katika jamii.
Dkt,Mzuri ameyasema hayo huko Tunguu
Wilaya ya kati Unguja katika ofisi za Chama hicho kufuatia uzinduzi wa ripoti
ndogo ambayo inatazama kwanamna gani vyombo vya habri vinawaandika ama
kuwaripoti wanawake viongozi katika habari za kila siku visiwani hapa.
Amesema kwa kuwa vyombo vya habari
vinanafasi kubwa ya kufanya mabadiliko wakati huu ikiwa ni kuandika na kuripoti
matukio mbali mbali yanayofanywa na wanawake viongozi Serikali n ahata wasiokua
viongozi ndani ya Serikali.
Amesema vyombo vya habari kupitia
mkakati maalumu wanawake kuwaandaa wanawake kushika nafasi za uongozi
kupitia vipindi vyao vya kila siku kwani wanawake ni watu wanaoitaji motisha.
Ameeleza kuwa kikawaida wanawake wengi
wamekua wakishindwa kusika nafasi za uongozi kutokana na kukosa maandalizi bora
ya kutaka kushika nafasi hizo badala yake wengi wao huamua kujitokeza kugombea
nafasi hizo bila kukosa maandalizi mazuri ya awali.
Akiendelea kufafanua zaidi Mkurugenzi
huyo alimtolea mfano Rais Samia Suluhu na kueleza kuwa ni mtu aliepitia hatia
hatua mbali mbali hadi kufika kuwa Rais na niwazi kwamba ni miongoni mwa
wanawake walioandaliwa na kujitengeneza vyema kushika nafasi tofauti mpaka kuwa
Raisi.
Akiwasilisha ripoti hio mkufunzi wa
maswala ya habari Dkt,Abuubakar Rajab alisema kupitia utafiti wake wa
vyombo mbali mbali vya habari vinavyofanya kazi visiwani hapa na Tanzania kwa
ujumla bado vimekua vikitoa nafasi ndogo sana kwa viongozi wanawake.
Amesema imekua kawaida kutoona habari
ianyomuhusu mwanamke kupewa kipao mbele kwenye magazeti au ata redio badala
yake wengi wao wanaamini kuwa wanaume ndio wanaopaswa kupewa kipao mbele kila
leo.
Kwa upande wake mratibu wa mradi wa
ushirikishwaji wanawake katika uongozi kutoka TAMWA-ZNZ Salma Amir
Lusangi alisema mradi huo wa miaka mine unalenga kuwawezesha wanawake elfu sita
kutoka wilaya 11 za Unguja na Pemba.
Amesema anaamini elimu watakayopatiwa
wanufaika wa mradi huo italeta tija hatimae wanawake wengi wataweza kushika
nafasi mbali mbali za uongozi iwe kwenye jamii zao au hata za kisiasa.
Mradi wa ushirikishwaji wanawake
katika nafasi za uongozi unatekelezwa na TAMWA-ZNZ chini ya ufadhili wa Ubalozi
wa Norway Nchini Tanzania.




0 Maoni