Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe:Ayoub Mohamed
Mahmoud ameishauri kamati ya Sensa ya Mkoa huo kuzingatia vipaumbele vya
huduma za Jamii watakapoanza
kuhesabu Watu na Makaazi yao.
Akizindua Kamati hiyo Ofisini kwake Mkokotoni Mhe:
Ayoub amesema sensa ni kwaajili ya ustawi wa
jamii hivyo kutozingatia
upatikanaji wa huduma za jamii ni kurejesha nyuma maendeleo ya wananchi.
Amesema Serikali imeamua kufanya Sensa ni kwaajili
ya kupanga huduma kwa jamii hivyo kushindwa kutambua huduma inayohitajika
Kwa Sehemu husika itasababisha Serikali
Kushindwa Kupanga Miundombinu ya huduma kwa sehemu hiyo jambo ambalo ni
kuwakosesha Wananchi kupata haki yao ya msingi.
Mjumbe wa kamati hiyo Ndugu Sabri Muhoma amesema
Sensa ya mara hii itakuwa na madadisi manne yatakayozingatia huduma za jamii,
idadi ya Kaya, Majengo Na Anuani Za
Makaazi hivyo amewataka
wananchi kujiandaa na sensa hiyo ili lengo la Serikali Lifanikiwe.
Sensa ya watu na makaazi inayotarajiwa kufanyika Mwaka 2022 Na Majaribio Ya Sensa Hiyo Itafanyika Tarehe 11 Mwezi Huu Na Kwa Upande Wa Mkoa Wa Kaskazini Unguja Shehiya Ya Kilindi Na Shehia Ya Bumbwini Misufini Zitahusika Na Sensa Hiyo Ya Majaribio.





0 Maoni