Waziri wa nchi ofisi ya Rais, Fedha na mipango Zanzibar, Jamal Kassim amesema Zanzibar imepata mgao wa sh. Milioni 971, laki nne, 69 elfu, 652 kutokana na makusanyo ya tozo ya miamala ya simu kati ya Julai 15 hadi 31 Mwaka huu.

Akizungumza na mwandishi wetu Ofisini kwake Vuga Mjini Unguja mhe. Jamal Kassim amesema mgao huo wa fedha unatokana na makusanyo ya jumla sh. bilioni 23.6 katika kipindi hicho cha wiki mbili zilizokusanywa Zanzbar.

Ameeleza fedha zilizozipata Zanzibar umeekwa kwenye mfuko maalumu kwa ajili ya miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa barabara za ndani kwa kiwango cha lami.

Mhe. Jamal amesema kuna muongozo maalumu unaosimamia namna ya kukokotoa fedha zinazokusanywa ili kupata mgao wa fedha hizo za makusanyo ya tozo kwa upande wa Zanzibar.

Aidha amewasihi wananchi kuendelea kutumia huduma za miamala ya simu ili kuchangia shughuli za maendeleo katika Taifa.