Timu ya Yanga imewapiku
mahasimu wao Simba baada ya kufanikiwa kuinasa saini ya kiungo wa Kimataifa
Raia wa Uganda Halid Aucho
Aucho alitua
hapa Nchini hivi karibuni kwaajili ya kuja kuzungumza na Viongozi wa Simba baada
ya kumpa Mualiko hata hivyo inaonekana Dili hilo halikufanikiwa
kwa sasa Aucho yuko
kwao Uganda akirejea karibuni kutoka hapa Tanzania baada ya Yanga kupindua Meza
ya Mahasimu wao na kumalizana na Mchezaji hyo
Dili la Aucho
kwa Simba huenda lilikwama kwa kile kilichoelezwa kuwa Jamaa alihitaji kiwango
kikubwa cha Mshahara jambo ambalo Yanga walifikia Makubaliano na Kumalizana nae
Akiwa kwao
Uganda, Aucho amethibitisha ni kweli alikuwa Tanzania lakini hakutaka kuweka
wazi ni timu ipi amemalizana nayo akisema klabu ndio yenye jukumu la kutangaza
usajili wake, ingawa habari za ndani zinaeleza kuwa Yanga tayari
wameshamalizana nae.





0 Maoni