Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Dkt.
Saada Mkuya, amesema atahakikisha haki za watu wenye ulemavu zinashughulikiwa
katika nyanja zote za maendeleo.
Akizungumza katika bonaza la shamra shamra za
kuelekea siku ya Vijana Duniani, lililofanyika Uwanja wa Amani Mjini Unguja,
amesema watu wenye ulemavu wanauwezo mkubwa wa kichumi na kiakili hivyo ipo
haja ya kupewa kipaombele.
Ameeleza kuwa, watu wenye ulemavu wanauwezo wa
kufanya shughuli mbali mbali za kijamii ambazo zinaweza kuwainua kiuchumi
ikiwemo michezo hivyo ni muhimu kupewa haki zao.
Aidha Dkt. Saada amesema watu wenye ulemavu wana uwezo
mkubwa wa kushiriki michezo mbali mbali kama wanavyoshiriki watu wengine hivyo
ni vyema yanapofanywa mabonaza washirikishwe ili waoneshe uwezo wao.
Nae Kaimu Mkurugenzi wa taasisi ya Madrasa Early
Childhood, Sharifa Suleiman amesema wameamua kuzielekeza jitihada zao kwenye
bonaza hilo, kwani wanaamini michezo ina manufaa makubwa katika kukuza afya ya
mwili, akili, kijinsia na kijamii.
Mwenyekiti wa Shirikisho la watu wenye ulemavu
Mwandawa Khamis amesema bonaza hilo limethibitisha wazi kuwa watu wenye ulemavu
wanauwezo wa kushiriki katika michezo mbalimbali kama binadamu wa kawaida.
Bonaza hilo lenye Kaulimbiu “michezo na lishe bora
kwa afya ya vijana wenye ulemavu” linahusisha michezo mbalimbali ikiwemo, riadha,
kuvuta kamba, kufukuza kuku, mpira na mchezo wa mpira kwa watu wasioona.





0 Maoni