Aliekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya ,Ustawi wa Jamii, Wazee ,Jinsia na Watoto Omar Dadi Shajak (kulia) akimkabidhi Katibu Mkuu Wizara ya Afya ,Ustawi wa Jamii, Wazee ,Jinsia na Watoto Dkt .Fatma Mrisho nyaraka na vitabu mbalimbali ikiwa ni ishara ya kumkabidhi Wizara hiyo rasmi ,hafla iliyofanyika  katika Ukumbi wa Mkutano wa Wizara ya Afya Mnazimmoja Mjini Unguja, katikati ni Waziri wa Afya ,Ustawi wa Jamii, Wazee ,Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui.
 

Na mwandishi wetu

Waziri wa Afya ,Ustawi wa Jamii, Wazee ,Jinsia na Watoto, Nassor Ahmed Mazrui amewataka watendaji wa wizara hiyo kufanya kazi kwa bidii ili kuendana na kasi ya awamu ya nane.

Hayo ameyasema katika hafla ya makabidhiano ya ofisi ya Katibu Mkuu yaliyofanyika Wizarani  hapo mara baada ya kuapishwa kwa Katibu Mkuu mpya waWizara hiyo

Mazrui amewataka watendaji kujitathmini ili waweze kuimarisha utendaji wa kazi, pamoja na  kurekebisha kasoro zinazojitokeza kwa lengo la kuleta ufanisi kazini.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa ofisi, Katibu Mkuu Wizara ya Afya ,Ustawi wa Jamii, Wazee ,Jinsia na Watoto Dkt Fatma Mrisho amesema atahakikisha kila mwananchi anapata huduma bora za afya katika maeneo yote ya mijini na vijijini.

Amewataka wafanyakazi kubuni mikakati itakayosaidia katika kuleta maendeleo ya sekta ya afya.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya ,Ustawi wa Jamii, Wazee ,Jinsia na Watoto Dkt .Fatma Mrisho akizungumza na watendaji wa Wizara ya Afya mara baada ya kukabidhiwa Wizara hiyo , hafla iliyofanyika  katika Ukumbi wa Mkutano wa Wizara ya Afya Mnazimmoja Mjini Unguja.

Waziri wa Afya ,Ustawi wa Jamii, Wazee ,Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui akizungumza na watendaji wa Wizara hiyo kuhusiana na mashirikiano mazuri baina yao na Katibu wa Wizara hiyo aliyeteuliwa hivi karibuni katika hafla ya makabidhiano ya Wizara iliyofanyika Ukumbi wa  Mkutano wa Wizara ya Afya Mnazimmoja Mjini Unguja.