Aliyekuwa Katibu Mkuu (OMKR) Khadija Kamis Rajab (kushoto) akimkabidhi nyaraka na vitabu mbalimbali Katibu Mkuu (OMKR) Omar Dadi Shajak (kulia) ikiwa na maana ya kumkabidhi Ofisi hiyo rasmi, hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Kilimani Mjini Unguja. Katikati ni Waziri wa Nchi (OMKR) Saada Mkuya Salum.

Na mwandishi wetu
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa  Rais Dr Saada Mkuya Salum amewataka wafanyakazi wa wizara hiyo kutekeleza vyema majukumu yao ili kufikia lengo lililokusudiwa na  Serikali la kutoa huduma bora kwa wananchi.

Ameyasema hayo huko katika ukumbi wa Ofisi hiyo iliyoko Migombani wakati wa makabidhiano ya Ofisi kwa Makatibu wakuu na kuwataka kushirikiana katika utendaji wa kazi na kuwakaribisha na kufanya kazi zao kwa ufanisi.

Amesema muelekeo wa kazi katika wizara hiyo unakwenda vizuri hivyo amewasisitiza kuwa nae karibu katibu mpya katika kutekeleza majukumu ya Serikali ambapo inahimiza kila mfanyakazi kufanya kazi zake kwa ufanisi.

Aidha amemshukuru katibu anaeondoka kwa alivyofanya kazi zake kwa na kumuomba anakokwenda akayatimize wajibu na uimara wake kama alivyoyafanya hapo.

Nae Katibu Mkuu Kazi na Uwezeshaji Khadija Khamis Rajab amesema kwa muda aliofanya kazi ameweza kupata mafanikio ikiwemo kupata ofisi ambapo hapo mwanzo kulikuwa kuna ufinyu na kuweza kupunguza baadhi ya madeni ya wafanyakazi yakiwemo wanayodai  Pesa za likizo na mambo mengineo.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamo wa kwanza wa Rais Omar Dadi Shajack ameahidi kufanya kazi kwa mashirikiano ili majukumu ya kazi yaweze kuendelea ikiwemo uwajibikaji kwa kila mmoja.