Mbunge wa Jimbo la
Uzini ambae pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe Hamis Chilo
amesema uzembe unaofanywa na baadhi ya watendaji unasababisha baadhi ya kesi za
udhalilishaji kuchukua muda kukamilika ushahidi wake jambo ambalo linawaumiza
wananchi
Mhe Chilo ameyasema
hayo jana(Augost 10) wakati akijibu malalamiko ya wananchi katika Mkutano wa hadhara
ulioitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Rashid Adid na kushirikisha
wananchi kutoka Shehia zote Nne za Jimbo la Uzini kwaajili ya kuskiliza kero za
wananchi na kuzipatia Ufumbuzi
Amesema hakuna sababu katika Kesi ya Mtoto
aliekutwa amedhalilishwa na upelelezi wake ukafika miezi sita au saba
wakati ushahidi uanonyesha wazi kuwa mtoto ameharibiwa.
‘‘unajua kuna mambo mengine kama kuna baadhi
ya watu wanazembea zembea, hakuna sababu kesi ya mtoto aliezalilishwa kesi ikafika
miezi saba au nane, wakati ushahidi upo maana umemkuta hasa mtoto ameharibiwa
ushahidi wote upo alafu unaendelea kupeleleza, kupeleleza et ushahidi
haujakamilika ,ushuhudie nini’’amesema Mhe Chilo.
Katika mkutano huo Mhe
Chilo amemuahidi Mkuu wa Mkoa kukaa na watendaji wa Jeshi la Polisi kwaajili ya
kuhakikisha wanazipatia ufumbuzi changamoto hizo.





0 Maoni