Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdullah anatarajiwa
kuwa mgeni rasmi siku ya Uzinduzi wa Wiki ya mwananchi iliyoandaliwa na Klabu
ya Yanga inayotarajiwa kuzinduliwa Asubuhi ya Jumapili Agost 22 2021
Sambamba na Sherehe nyengine Uzinduzi huo pia utahusisha Dua ya kumuombea
Muasisi wa Klabu hiyo ambae pia ndie Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar.
Akizungumza na Wanahabari jijini Dar es Salaam,
Mwenyekiti wa Kamati ya Habari na Hamasa, Qs. Suma Mwaitenda amezema Uzinduzi
huo wa Wiki ya Mwananchi utaambatana na shughuli mbalimbali za Kijamii
zikazofanywa na Wana Yanga Sc na viongozi wa Yanga Sc.
"Tutakuwa na shughuli za kijamii kuanzia Jumamosi (leo), tunatarajia kuwa tutatoa
msaada wa mgodoro katika Hospitali za Mnazi Mmoja na Mwemberadu, lakini
Jumapili ndio utakuwa uzinduzi rasmi ambao utafanyika baada ya dua maalum ya
kumuombea muasisi wetu, Hayati Sheikh Abeid Aman Karume," amesema.
Amesema Jumapili Wana Yanga Sc watakusanyika ofisi
za Yanga Sc Kariakoo Zanzibar na kisha
kufanya matembezi ya mshikamano kwenda Ofisi ya CCM Kisiwandui lilipo kaburi la
Marehemu Karume ambapo itafanyika Dua
"Katika matukio yote ya Dua na baadaye Uzinduzi
kwenye ukumbi wa ZSSF mgeni wetu tunataraji atakuwa Makamu wa Pili wa
Rais," amesema.
Katika hatua nyingine, Qs. Suma Mwaitenda
ameishukuru Kampuni ya Azam Marine and Kilimanjaro Fast Ferries kwa kujitokeza
kuwa mmoja wa Wadhamini wa Wiki ya Mwananchi mwaka huu.




0 Maoni