Vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia kwa
watoto vimeelezwa kuongezeka kisiwani Zanzibar kwa Mwezi Julai hali
inayotishia ustawi wa watoto.
Mtakwimu Ramla Hassan Pandu kutoka afisi ya mtakwimu
mkuu wa Serikali kitengo cha makosa yajinai, madai na jinsia amesema jumla ya
matukio 108 ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia yameripotiwa ndani ya mwezi
wa Julai 2021 idadi ambayo imeongezeka ikilinganishwa na mwezi wa Mei 2021
makosa 97.
Amefahamisha kuwa, Wilaya ya Magharibi A imeripoti
makosa 29 ambayo ni mengi zaidi kwa mwezi Julai ikilinganishwa na Wilaya
nyengine ikifuatiwa na Magharibi B (23).
Nae Mkurugenzi Jinsia na Watoto kutoka Wizara ya
Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto, Nasima Chum amesema kumezuka
wimbi la utoroshaji wa watoto wa kike kuanzia miaka 14 na 17 hivyo ni vyema
wazazi kuhakikisha wanawasimamia ipasavyo kwa kutambua nyendo zao kwa kuanza
kuzuia na sio kuondosha.
Nae wakili wa Serikali, Khamis Othman kutoka afis ya Mkurugenzi wa
mashtaka amesema vitendo vingi vya udhalilishaji vinachochewa na utumiji wa madawa ya kulevya kwa
vijana hivyo huchangia kufanya vitendo
vya udhalilihsaji




0 Maoni