Na Suleiman Mohamed
Waziri wa Maji
na Nishati Zanzibar Mh Slemani Masood Makame amesema Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar imelenga kuondosha Changamoto ya upatikanaji wa Maji safi na
salama kwa wananchi wa maeneo yote hasa
katika maeneo ya Makazi na uwekezaji.
Mhe Sleman ameyasema
hayo kiwekwanga Wilaya ya Kaskazini B Mkoa wa Kaskazini Unguja, wakati wa
Uzinduzi wa Kikundi cha Baba lishe na Mama lishe wa Kijiji cha Kiwengwa
mafarasi ambapo wanakikundi hao walilalamikia changamoto ya upatikanaji wa maji
.
Amesema Serikali
itapita katika maeneo yote yenye changamoto ya upatikanaji wa maji safi na
salama na kubaini kasoro zilizopo ili waweze kuzifanyia kazi kwaajili ya
kuhakikisha maji safi na salama yanapatikana katika maeneo yote ya Zanzibar ikiwemo
Kiwengwa.
Kuhusiana na
kikundi hicho Mhe Sleman amesema yuko
tayari kushirikiana na mwakilishi wa Jimbo hilo kuhakikisha wanatoa msaada wa
kukiweshesha kikundi hicho kisajiliwe ili waweze kunufaika na fursa mbali mbali
Serikalini ikiwemo mikopo kwaajili ya kuendeleza kikundi.
Nae Mwakilishi
wa Jimbo la Mahonda Asha Abdallah Mussa
amesema atahakikisha anaishauri Serikali ili mfuko wa uwezeshaji Kiuchumi
kutoka Wizara husika unasimamiwa ipasavyo ili uweze kuwanufaisha wananchi kama
lengo lilivyokusudiwa.
Awali akisoma
risala kwa niaba ya wanakikundi cha Baba lishe na Mama lishe Mariamu Juma
(kitam) amesema changamoto inayowakabili kikundi hicho ni Upatikanaji wa Maji
safi na Salama kwaajili ya kuendeleza biashara zao hali inayopelekea kununua
Dumu moja la Maji kwa shilingi elfu moja (1000)
jambo walilolieleza linarudisha nyuma juhudi zao.
Katika hafla
hiyo Mwakilishi wa Jimbo hilo Asha Abdallah Mussa ametoa kiasi cha shilingi
laki Tano taslim (500,000) kwaajili
ya kikundi hicho chenye wanachama zaidi ya hamsini tokea kuanzisha kwakwe mwezi
june 2021.
Mwakilishi jimbo la mahonda akimweleza jambo Mgeni Rasmi Mh Sleman Masood





0 Maoni