Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkiritiki akipata Chanjo ya Uvico 19

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti  leo (04.08.2021) amewaongoza wananchi wa Mkoa huo kupata chanjo ya kinga dhidi ya Ugonjwa wa Virusi vya Corona ambapo amesema kuwa chanjo hiyo ni Salama na inalenga kuwasaidia watu kuwa na kinga imara .

 Amesema Wananchi wa Mkoa wa Rukwa ni vema wakajitokeza kupata chanjo jiyo dhidi ya Ugonjwa wa Virusi vya Corona ambapo Serikali Mkoa wa Rukwa imeanza kutoa chanjo kwa wananchi wenye uhitaji wa Chanjo hiyo kwa hiyari.

 Mkiritiki amewaeleza wakazi wa Sumbawanga waliokusanyika kwenye hospitali  ya Rufaa ya Mkoa Sumbawanga kuwa Serikali ya Awamu  ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imethibitisha pasipo shaka kuwa chanjo hii ya UVIKO  19 ni salama na kuwataka wengi wajitokeze kupata chanjo hiyo.

 "Rais Samia amesema chanjo hii ni bure na ya hiari kwa mwananchi yeyote mwenye kuhitajinili kujikinga na ugonjwa wa Corona. Mimi leo nitakuwa wa kwanza kuchanja hapa hapa " alisema Mkirikiti

 Akizungumza kuhusu chanjo hiyo Mganga Mkuuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Boniface Kasululu  alisema lengo la serikali  kutoa dozi hizo za chanjo ya kinga dhidi ya ugonjwa wa virusi  vya Corona utasaidia kuongeza kinga ya mwili ya mwanadamu .

 Aliongeza kusema lengo jingine ni kupunguza gharama za matibabu kwa wagonjwa pia kupunguza idadi ya vifo vinavyotokana na virusi vya Corona.

" Tumepokea dozi za chanjo Elfu Ishirini ambazo tayari zimefikishwa kwenye vituo 11 vilivyoanishwa kutoa chanjo, wananchi naomba tujitokeze kupata chanjo" alisema Dkt. Kasululu 

 

baadhi ya Wanachi waliojitokeza kupata Chanjo ya Uvico 19 Katika Hospitali ya Mkoa Sumbawanga