Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja Rashid akizungumza na wananchi wa Jimbo la Uzini Wilaya ya  Kati,Mkoa wa  Kusini Unguja

Na mwandishi wetu

Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja Rashid Hadid amesema Serikali ya Mkoa imedhamiria kushuhulikia kikamilifu changamoto zinazokabili Mkoa huo ikiwemo uuzaji na utumiaji wa madawa ya kulevya, wizi wa mazao na suala ya udhalilishaji

Mhe Hadid    ametoa kauli hiyo jana (August 10)  katika Shehia  kiboje Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja alipokutana na wakaazi wa Shehia Nne za Jimbo la Uzini  kwa ajili ya kusikiliza kero zinazowakabili katika vijiji vyao ambapo amesema hadi sasa tayari ameshapata orodha ya majina ya wauzaji na watumiaji wa madawa ya kulevya na amedhamiria kuwachukulia hatua za kisheria wale wote waliohusishwa katika ripoti yake.

 Katika hatua nyengine Mh Hadid Amesem Serikali haitasita kuendelea  kuyafanyia uchunguzi   majina ya watu wa jimbo la  uzini ambao wanajihusisha na vitendo vya  udhalilishaji na wizi wa mazao.

Amesema Jambo la udhalilishaji ni baya hivyo ni vema wananchi wakashilikiana na Viongozi wa Serikali ikiwemo Masheha katika kujenga nidhamu na Maadili mema katika Jamii

Kwaupende wao Mwakilishi na Mbunge wa Jimbo hilo amemweleza mkuu wa mkua juu ya kufahamu          changamoto zinazokabili Jimbo hilo na kuahidi kushirikiana na wananchi katika kupata ufumbuzi wa changamoto hizo

Katika kushuhulikia changamoto hizo kwa Vitendo Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja ametoa wito wa kuundwa kwa Kamati za Ulinzi shirikishi katika shehia ili kushirikiana kwa pamoja kuondoa changamoto zinazokabili Jimbo hilo.