Hospital ya Rufaa ya Mnazi Mmoja imeeleza kukabiliwa na ongezeko la wagonjwa wa Covid 19 Hospitalini hapo hali inayosababisha uwepo wa changamoto ya uhitaji  mitungi ya gesi ya Oksjeni zaidi kutokana na  ongezeko la Wagonjwa hao wa Covid 19.

Akizungumza na sknews kwa njia ya simu Msemaji wa Hospitali ya Mnazi mmoja Hassan Makame amesema Jumla ya Mitungi Mia Nne (400) inahitajika ili kukabiliana na mahitaji wa wagonjwa waliopo hivi sasa.

Amesema mitungi ya Oksijeni kwa sasa imekua ikiwalazimu kuagiza  kutoka Dar es salaam kutokana na hospitali hiyo mtambo wake wa kuzalisha mitungi hiyo kutokidhi kwakua uzalishaji wake ni mitungi 30 kwa siku idadi ambayo ni ndogo ukilingalisha na mahitaji ya Wagonjwa.

" kwa sasa mitungi tulionayo  haizidi mia mbili na kidogo na sisi hapa tunatumia mitungi mia kwa siku, tunahitaji walau kama hatuna mingi tupate mitungi walau mia nne''

Hassan Makame amesema licha ya Mtambo wa Hospitali hiyo kuwa  na uwezo wa kuzalisha idadi ndogo ya Oksijeni lakini mtambo huo pia umeshaanza kuchakaa kwa sasa hali ambayo mbeleni itachangia kushindwa  kuleta ufanisi.

amesema kutokana njia pekee ya kuondoa tatizo hilo ni kupatiwa kwa mtambo wa kisasa unaozalisha hewa ya Oksijeni kutokana na kuongezeka kwa mahitaji hayo kila siku.