Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 04 Agosti, 2021 amemteua Bi. Mtumwa Khatib Ameir kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).

 Bi. Mtumwa Khatib Ameir ni Afisa Mtendaji Mkuu na Msimamizi wa Hakimiliki Zanzibar.

 Uteuzi huo unaanza leo tarehe 04 Agosti, 2021.