Mtoto mmoja mwenye umri wa miaka 11, anaeishi Shehia ya Finya Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba, amekutwa amejinyonga  ndani ya chumba chao kwa kutumia Khanga

Akizungumza na Sknews  Mkuu wa Wilaya ya Wete Mgeni Khatib Yahya  amesema tukio hilo limetokea jana (Agosti 24) majira ya saa 12 jioni katika shehia ya Finya ambapo hadi sasa Chanzo cha tukio hilo hakijajulikana.

Bi salma amesema mtoto huyo anaaejulikana kwa jina la Hildat Mohamed Seif anasoma Darasa la Nne katika Shule ya Msingi Finya ambapo siku ya tukio majira ya saa 10 za join  Mtoto huyo alikwenda skuli kwa ajili ya masomo ya ziada na aliporudi majira ya saa 12 aliingia ndani baada ya muda akakutwa amejinyonga.

‘‘kiukweli chanzo cha tukio bado hakijajulikana ila huyo mtoto anaishi na mama yake ambae kwa kweli nimjamzito kama si wakujifungua leo basi kesho, baba wa mtoto siku ya tukio hakuwepo Kijijin hapo kwahyo hakukua na mtu aliekua akifuatilia nyendo za mtoto ’’ amesema bi Mgeni

Amesema kwa mazingira kwa jinsi ya livyo yanaonesha wazi huenda mtoto huyo amejinyonga  ingawa bado polisi wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha tukio lenyewe

‘‘mazingira kwa jinsi yalivyo inaonesha huenda mtoto amejinyonga maana pale eneo la tukio linaonesha mtoto alipanda kitandani akajifunga khanga shingoni na kuitupa khanga kwenye Dari hali iliyopelekea kumkaba shingoni na kusababisha kifo chake’’