Na mwandishi wetu
Mkuu wa wilaya ya
Mjini Rashid Simai Msaraka ametoa wiki moja kwa wafanyabiashara wa
vifaa mbali mbali wa maeneo ya Mlandege Mjini Unguja, kuondoa sehemu ya
mapaa ya maduka yao yaliyozidi pembezoni mwa barabara na kusababisha kero
kwa Wananchi
.Akizungumza na
wafanyabiashara hao, Mkuu wa wilaya amesema kwa sasa maduka
hayo yamekuwa yakileta usumbufu kwa wanaokwenda kwa miguu na hata
wale ambao wanaopaki gari zao hali inayoweza kusababisha ajali kwa wananchi .
Amesema endapo
wafanyabiashara hao wataondoa sehemu ya mapaa yaliyozidi kunaweza kupatikana nafasi kubwa ya waendao kwa miguu na hata
sehemu ya kupaki Magari na kuondoa msongamano wa magari katika maeneo hayo.
Nao baadhi ya
wafanyabiashara wa maeneo hayo, wameiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
kuwapa muda wa wiki moja kwaajili ya kufanya matayarisho ya kuondoa vifaa vyao
katika maduka hayo kwa kuwa kwa sasa hawajiandaa kutafuta maeneo mengine.
Aidha wafanyabiashara
hao wamesema kuwa wapo tayari kufuata maagizo yaliyotolewa na
serikali na kuhakikisha kuwa watabomoa vipaa hivyo ili kuondosha usumbufu
unaojitokeza mara kwa mara kwa watu wanaotumia maeneo hayo.





0 Maoni