Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Salama Mbarouk ameitaka jamii kuzitumia vyema rasilimali za bahari pamoja na kuzilinda ikizingatiwa ni vyanzo muhimu katika kuelekea uchumi wa buluu na ukuaji wa uchumi wa nchi.
Ushauri huo umetolewa kwa niaba yake na Mkuu wa
Wilaya ya Micheweni, Moh’d Mkobani wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uhifadhi wa
Matumbawe inayotekelezwa na Jumuiya ya Kwanini Foundation, amesema matumizi sahihi
ya rasilimali za bahari huchochea ukuwaji wa uchumi wa nchi na wananchi.
Nao Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kwanini Foundation pamoja
na Mkuu wa Doria za bahari kutoka Wizara ya Uchumi wa Buluu wamesema kampeni
hiyo itasaidia kuongezeka mazao ya baharini ikiwemo samaki.
Awali Afisa Mdhamini wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais,
Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Thabit Othamna
amezitaka asasi za kiraia kuendelea kushirikiana na Serikali kutatua changamoto
zinazowakabili wananchi.




0 Maoni