Mbumge wa viti maalum kundi la Wanawake Mkoa wa Kaskazini Pemba Asya Sharif Omar ametoa wito kwa wachezaji soka kuutumia vyema muda wao kufanya mazoezi kwani soko la soka duniani liko wazi na kila uchao linahitaji kwachezaji wenye uwezo na vipaji .
Pia alisema kutokana na dunia kuwa kijiji kimoja ,
mchezaji mwenye uwezo wa soka, nidhamu na anayejituma ni rahisi
kununuliwa toka mahali popote duniani kwa bei kubwa akatajirika.
Asya ambaye ni mwanamichezo ameyaeleza hayowakati
akizungumza na Mwandishi wetu kuhusuiana na mtazamo wake katika Masuala ya
ajira kwa vijana kupitia soka.
Amesema ni vema wazazi wakawapa nafasi vijana kuishi
katika ndoto wanazoziamini kwakua mpira
wa miguu pamoja ni afya na burudani lakini mpira sasa imekua sehemu inayoajiri
watu wengi na mafanikio yake ni yamuda mfupi
soka la sasa lina soko kubwa hivyo linatafuta bidhaa
ambayo ni wachezaji wenye uwezo vipaji na uhodari ili wananunuliwe
na timu kubwa za soka duniani.
amesema iwapo wachezaji wa Soka Visiwani Zanzibar watatilia
maanani kufanya mazoezi kwa bidii, kujituma na kufuata maelekezo ya walimu
anamatumaini makubwa ya kuona Zanzibar ikizalisha wanamichezo wengi
watakaotumika katika timu ya Taifa na Vilabu mbali mbali Nchini na Nje ya Nchi.
"Nichukue nafasi kuwataka wachezaji wa
soka wajitambue na kuelewa soka la sasa duniani ni bidhaa muhimu.Ni
bidhaa isiokosa soko kwani inahitajika kila uchao duniani. Iwapo wachezaji wa
timu zetu watajituma soko la kandanda litawafuata hapa hapa Pemba "Alisema
Asya





0 Maoni