JAMII imehimizwa kutenga muda   kwa ajili ya kufanya mazoezi ili kulinda afya zao na kuepukana na maradhi nyemelezi  ambayo matibabu yake yangehitaji kutumia fedha nyingi.

 Akizungumza na vikundi vya mazoezi vya Mikoa miwili ya Pemba, baada ya kushiriki mazoezi hayo yaliyofanyika kwenye viwanja vya Polisi Konde, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba  Salama Mbarouk Khatib amesema mazoezi husaidia kujenga mwili na  pia tiba   ya maradhi nyemelezi.

 Amesema ufanyaji wa mazoezi unapunguza uwepo  wa maradhi ya  mbali mbali ikiwemo presha na kisukari.

 Meneja wa benki ya NMB Tawi la Chake Chake Hamad Mussa Msafiry ametumia fursa hiyo kuwaomba wanavikundi kujiunga na bima a vikundi vinavyotolwa na benki hiyo.

 Amesema  kupitia utaratibu huo wa bima wanavikundi wanaweza kunufaika na hivyo kuboresha hali zao kiuchumi.

 Akisoma risala Katibu wa Kikundi ha Kichungwani Fitness Club Rajabu Said amesema uwamuzi wa kuanzisha kikunid hicho cha mazoezi ni moja ya mikakati yao ya kuboresha afya zao.