Afisa Mtendaji Mkuu wa
Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela), Godfrey Nyaisa
akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tano ya maafisa Biashara
kutoka mikoa ya Morogoro, Dodoma na Singida, jijini Dodoma Agosti 16,
2021.Na mwandishi wetu
Serikali ya
Jamhuri wa Muungano wa Tanzania iko
mbioni kunzisha mpango wa malipo ya maombi ya biashara kwa njia ya
mtandao kwa lengo la kupunguza usumbufu kwa wapokea huduma.
Mpango
huo umetangazwa rasmi hii leo Augost 17 na Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa
Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) Godfrey Nyaisa wakati
akifungua mafunzo ya siku tano ya maafisa Biashara kutoka
mikoa ya Morogoro, Dodoma na Singida, jijini Dodoma.
Amesema
kuwa lengo la mpango huo ni kurahisisha utendaji Kazi na kuwadhibiti
maafisa wabadhilifu wa fedha za umma ambao baadhi
walikuwa wanajitengenezea vitabu feki vya leseni.
Nyaisa
amesema kuwa hivi sasa maombi yote ya leseni yatakuwa kwenye mfumo mmoja
ambapo mfanyabiashara atakuwa anaomba leseni kupitia kwenye mtandao
na kulipia kwa kutumia namba maalumu ya malipo serikalini (Control Number)
na kwamba mpango huo utapunguza kwa asilimia kubwa ubadhirifu hivyo
kuongeza wigo wa mapato.
"Serikali
ina shida na mfanyabiashara na mfanyabiashara ana shida hivyo msikurupuke
kuwafungia biashara, kaeni muelewane, mtumie busara lakini pia mkae
mkijuwa kuwa licha ya Serikali kutaka mapato lakini kazi yake kubwa
ni kutoa huduma," amesema Nyaisa.




0 Maoni